ZITTO AANIKA UHUSIANO WAKE NA DIVA


KWA mara ya kwanza Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe ameibuka na kuzungumzia uhusiano wake na mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi ‘Diva’ na kufuta uvumi mzito uliokuwa ukizagaa kuwa wawili hao ni wapenzi.

Zitto alifunguka hayo juzi kupitia kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Televesheni ya East Africa ambapo alikanusha kuwa hana uhusiano wowote wa mapenzi licha ya kudaiwa kutungiwa wimbo na mtangazaji huyo kama ishara ya penzi lao.“Mh! Kama yeye amenitungia wimbo sijui lakini mimi sina uhusiano naye wowote wa kimapenzi,” alisema Zitto.
Katika mahojiano hayo, mheshimiwa huyo alifungukia skendo nyingine inayomhusisha kutembea na staa wa Bongo Fleva, Mwasiti Almasi na kudai hakuna ukweli wowote juu ya ishu hiyo.
Previous
Next Post »