KAJALA AZINDUA MUVI YAKE YA ‘MBWA MWITU’

2Msanii wa filamu Tanzania, Kajala Masanja aka Kajala siku ya jana ameizundua muvi yake ya ‘Mbwa Mwitu’ katika ukumbi wa Cinema Mlimani City.
Hakika ni short film ila imejaa ujumbe mzito, wenye kusisimua na kuelimisha jamii kwa maovu ya yanayotokea hususani kwa vijana wengi wao wana umri usiozidi miaka ishirini, filamu hiyo ina kila sababu ya jamii kujifunza kwa kile kinachoonekana kwenye muvi ya ‘Mbwa Mwitu’.
Kupitia Kajala Entertainment imeweza kuchukua nafasi ya kutengeneza muvi hiyo kuonesha jinsi gani wananchi wanavyokosa amani ndani ya nchi yao kutokana makundi yanayo kosesha amani kwenye mitaa makundi hayo kama Panya Road, Bad Face na Mbwa Mwitu,.
Uzinduzi huo ulijaa na mastaa wengi sana wa tasnia tofauti tofauti za hapa Bongo, hakika kila mmoja aliyehudhuria uzinduzi huo amepata kuona jinsi gani makundi hayo yanavyotishia amani, na sasa huo ndiyo ujumbe tosha uliyotufikia wananchi, na kupitia kampuni ya ‘Kajala Entertainment’ imeweza kuwatafuta baadhi ya wahusika ambao waliokuwa wanafanya matukio kama hayo na kwa sasa wameacha kabisa na kuanzisha miradi yao.
Previous
Next Post »